Maisha ya mchuuzi aliyemuuzia Uhuru peremende za KSh 40 yadaiwa kubadilika

- Wachira alimuuzia Uhuru peremende wakati wa kampeni za marudio ya uchaguzi wa Oktoba 26, 2017 katika soko la Barma - Alimtembelea Katibu katika Wizara ya Usalama wa Ndani Karanja Kibicho na kulipwa deni hilo kwa niaba ya rais

- Wachira alimuuzia Uhuru peremende wakati wa kampeni za marudio ya uchaguzi wa Oktoba 26, 2017 katika soko la Barma

- Alimtembelea Katibu katika Wizara ya Usalama wa Ndani Karanja Kibicho na kulipwa deni hilo kwa niaba ya rais

- Aidha, Wachira alisema kuwa biashara yake imezorota sana kwani watu wamekuwa wakikataa kununua peremende zake wakidai alipewa pesa nyingi na Uhuru

Madai yameanza kuibuka kuhusu Dennis Wachira mchuuzi aliyemuuzia Rais Uhuru Kenyatta peremende za KSh 40 kwenye barabara ya Jogoo jijini Nairobi bila kulipwa.

Maisha ya Wachira ambaye alimrai Uhuru kupitia mtandao wa kijamii amlipe deni lake ili aweze kuimarisha biashara yake na hatimaye kulipwa deni hilo, yamedaiwa kuimarika zaidi tofauti na awali na sasa inadaiwa alipewa kitita kizuri.

Habari Nyingine: Mlinzi wa Uhuru aonekana na mkono bandia kwenye mpango wa siri wa usalama

Tuma neno ‘NEWS’ kwa 40227 ili kupata habari muhimu pindi zinapochipuka

Ijumaa, Desemba 14, Wachira alimtembelea Katibu katika Wizara ya Usalama wa Ndani Karanja Kibicho na kulipwa deni hilo kwa niaba ya rais.

"Kabla tuanze kuzungumza, nataka kukulipa deni lako la KSh 40 ambalo Rais Uhuru Kenyatta hakukulipa baada ya kununua peremende kutoka kwako, na ninataka unirudishie bakishishi ya KSh 10," Kibicho alisema huku akimpatia noti ya KSh 50.

Habari Nyingine: Mwanamke wa Kihindi akamatwa kwa kuanika paja lake kwenye mtandao wa Facebook

Katika mazungumzo yao ndani ya ofisi hiyo, Kibicho na mgeni wake walijadiliana mambo kadhaa yakiwemo ni kitu kipi hasa alichotaka rais amfanyie.

Awali TUKO.co.ke iliripoti kuwa, Wachira alisema angependa apawe kazi serikalini, lakini kwa sababu ya afya yake, hawezi kufanya kazi nzito.

Aidha, Wachira alisema kuwa biashara yake imezorota sana kwani watu wamekuwa wakikataa kununua peremende zake wakidai alipewa pesa nyingi na Uhuru.

Habari Nyingine: Jamaa amfurusha mkewe siku 2 baada ya harusi, adai mtu aliifungua 'sava'

"Tangu nilipomuuzia Rais peremende, biashara yangu haijakuwa ikifanya vema kwani watu wengi huamini kuwa maisha yangu yalifaa kubadilika, hawanunui hata bidhaa zangu," Wachira alisema.

Wachira alimuuzia Uhuru peremende wakati wa kampeni za marudio ya uchaguzi wa Oktoba 26, 2017 katika soko la Barma.

Lakini baada ya siku kadhaa tangu kualikwa katika ofisi ya Kibicho, huenda mambo yameanza kumnyookea kufuatia madai eti maisha yake ni bora kwa sasa.

Habari Nyingine: Ukweli kuhusu video ya mahaba inayodaiwa kunaswa Imenti House, Nairobi

Ingawa hamna ushahidi wowote kuthibitisha hilo, TUKO.co.ke imeng’amua kuwa, mtandaoni watu wanaendelea kudadisi na kuulizana maswali ikiwa kweli maisha yamembadikilia.

Wakati akijadiliana na Kibicho, Wachira alisema lengo lake ni kuona maisha ya familia yake yakiimarika kwa sababu inaishi katika ufukara mkubwa.

Habari Nyingine: Raila Junior amshambulia DP Ruto kuhusiana na katiba ya sasa

TUKO.co.ke inafuatilia matukio na yakijiri itakufahamisha zaidi lakini inamtakia Wachira na familia yake kila la heri na mafanikio tele hata wakati akiendelea na kazi yake ya kuuza peremende.

Una taarifa motomoto au sakata ambayo ungependa tuichapishe? Wasiliana nasi kwa news@tuko.co.ke, mwangi.muraguri@tuko.co.ke , kwenye WhatsApp: 0732482690 na kwenye Telegram: Tuko News

Chanzo: TUKO.co.ke

ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2BvzmeinmdiboF0g5VmpJqho52ubsXAZqScoKWqx6p5wKWgsp2dqsK7tcBmrKGtoqp6sbHRnqSeppSaerutjKSqoWVkZXq6rcOaoLCZXaDCo63DoqOio5FjtbW5yw%3D%3D

 Share!