Sigalagala: Mzee Amkomesha Kijana Wake Kuchumbia Kisura Fulani

Buda mmoja kutoka eneo la Sigalagala kaunti ya Kakamega aliwaduwaza wengi baada ya kumzomea mwanawe akimtaka akome kumchumbia binti ya mpango wake wa kando. Inaarifiwa kwamba mzee alichukua hatua hiyo akihofia kutemwa na mamake mrembo huyo ambaye walikuwa wamechumbiana kwa muda mrefu.

  • Inaarifiwa kwamba mzee alichukua hatua hiyo akihofia kutemwa na mamake mrembo huyo ambaye walikuwa wamechumbiana kwa muda mrefu
  • Mzee alimuonya mwanawe kwamba kipusa alikuwa na uhusiano wa karibu na familia yao na alifaa kumchukulia kama dadake

Buda mmoja kutoka eneo la Sigalagala kaunti ya Kakamega aliwaduwaza wengi baada ya kumzomea mwanawe akimtaka akome kumchumbia binti ya mpango wake wa kando.

Inaarifiwa kwamba mzee alichukua hatua hiyo akihofia kutemwa na mamake mrembo huyo ambaye walikuwa wamechumbiana kwa muda mrefu.

Kwa mujibu wa Taifa Leo, mzee alimuonya mwanawe kwamba kipusa alikuwa na uhusiano wa karibu na familia yao na alifaa kumchukulia kama dadake.

“Nimepata fununu kwamba wewe na msichana fulani mnachumbiana. Sitaki kusikia hayo mambo tena. Huyo ni dadako,” jamaa alikanwywa.

Semasema zinaarifu kwamba lofa alibaki kinywa wazi asijue la kusema.

“Mimi na huyo msichana tunapendana. Tumeshaweka mipango ya kuoana. Nachojua sina uhusiano wowote na yeye,” jamaa alimueleza babake.

Inasemekana kwamba semi za jamaa zilimsinya mzee sana.

Pia soma

Jamaa Afuta Harusi Yake na Binti Mwokovu Baada ya Video Akisakata Densi Klabuni Kusambaa

“Lazima uniheshimu kama mzazi wako. Iwapo hutaki kufuata mawaidha yangu tafuta pa kuishi,” mzee aliwaka.

Majirani walibaki kutazama sinema ya bwerere bila kuingilia kati.

“Huyu mzee naye aachane na kiaja wake. Mambo yake tunayajua. Yeye aendelee kula kuku amuachie mwanawe kifaranga,” jirani mmoja alisikika akisema.

Lofa anasemekana aliapa kutovunja uhusiano wake na mrembo huyo.

“Ukoo wangu na huyo msichana ni tofauti kabisa. Mimi sioni mahali huo ukoo wetu unapotokea. Mimi sirudi nyuma kabisa na siachani naye,” jamaa aliapa.

Duruu zinasema kwamba mzee alitishia kumchukulia hatua kali jamaa iwapo ataendelea kumchumbia msichana huyo.

“Naona umeamua kunipuuza. Sioni tukiishi na wewe hapa. Nakupa siku mbili ufanye uamuzi,” mzee alimfokea polo.

Vicheko vilisikika kutoka kwa majirani. Wengine walisikika wakimhimiza jamaa kutolegeza kamba.

“Huyo mzee ni mkora. Hakuna uhusianio wowote wa kifamilia au ukoo,” majirani walimzomea.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia news@tuko.co.ke au WhatsaApp: 0732482690.

Pia soma

Thika Mjini: Mrembo Aona Moto Kunyemelea Mume wa Dadake

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke.

Subscribe to watch new videos

Chanzo: TUKO.co.ke

ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2BvzmeinmdkZ4Zyf5ZmqqKfkaGuqK3LmmSmspWaeqK5yqiknquYlnqstcmapZplp5a4pnnKrpqhrZ2XtqJ5yqKqrqqRYrO2uMCnoGegpKK5

 Share!